SHIBE LiNAPUNGUA KILA KUCHAO
Mbona niseme shibe linapungua kila kuchao?? Kwa nini nikaangazia tu shibe ,ni kwa sababu bila chakula binadamu Hana uhai Tena. Sasa hivi kilichokuwa Cha Bei ya chini ni Cha Bei ya juu iliyo maradufu ,Bei ambayo hairidhishi ,Wengi wanaulizana tufanye nini ,twende wapi ,tumlilie nani. Bei ya mafuta ya kupika haswa ndio kizungumkuti kwa sasa ,vitoe si vitoe Tena kwani havina ladha kwa sababu havipati mafuta ya kutosha, usafiri nao kwa upande wao umesema "wakipandisha tutapandisha" nauli unaenda kupanda kwa kiwango Cha ajabu sana ,Wengi watalazimika kutembea kwa mguu hata ikiwa safari ya Marekani. Athari ya kupanda kwa Bei ya bidhaa hapa nchini inamkosesha mwananchi usingizi ,hajui kesho atakula nini pamoja na wanae ,lawana zinawapata wazazi kwa kuwa tu watoto wao hawajapata Cha kuweka mdomoni ,itafikia wakti binadamu ataamua kumla binadamu mwenziye kwani yeye ndo chakula kilichobakia mbele na nyuma. Niulize tu ila kwa unyenyekevu ,uliyemchagua atetee maslahi yako Yuko wapi ?? U...